Chuo Kikuu cha Makerere wakati wa machweo
10–13 Disemba 2026 · Kampala
CHAUKIDU
×
Chuo Kikuu cha Makerere

Kongamano la Kimataifa

la 11 la

Kauli Mbiu 2026

Twen’zetu Makerere! Lulu ya Afrika Yaita. Upo?

CHAUKIDU2026

"Kiswahili na Lugha Nyingine Afrika: Mustakabali wa Ndani na Nje ya Mipaka ya Darasa katika Dunia Inayobadilika"

Chuo Kikuu cha Makerere 10–13 Disemba 2026 Kampala, Uganda
Kongamano linafunguliwa baada ya
--
Siku
--
Saa
--
Dakika
--
Sekunde
Chuo Kikuu cha Makerere — minara ya kihistoria juu ya kilima
Nembo ya Makerere
Tangu 1922
"We Build for the Future"
Taasisi Mwenyeji

Chuo Kikuu cha
Makerere

Ungana nasi katika kitovu cha elimu cha Afrika Mashariki. Makerere inatoa mazingira ya kipekee ya kitaaluma kwa ajili ya mjadala mpana kuhusu mustakabali wa lugha ya Kiswahili duniani.

1922Kuanzishwa
35K+Wanafunzi
#1Afrika Mash.
Kuhusu Makerere
Kuhusu Kongamano Hili

Kutana na wataalamu, wakereketwa, na wadau wa Kiswahili toka sehemu mbalimbali Duniani.

Utafurahi kutangamana na Waswahili wengine na kuwa sehemu ya familia kubwa ya wasemaji wa Kiswahili Duniani! Mada kuu ni “Kiswahili na Lugha Nyingine Afrika: Mustakabali wa Ndani na Nje ya Mipaka ya Darasa katika Dunia Inayobadilika.” Jioni ya tarehe 12 Disemba, kutakuwa na tamasha kubwa la Utamaduni wa Mswahili, ambapo watu wote wanakaribishwa, hata wale ambao hawakushiriki katika kongamano.

Kamati ya maandalizi inaangalia uwezekano wa kuandaa shughuli za kitalii. Wale watakaohitaji kushiriki katika utalii watajulishwa gharama zitakuwa kiasi gani na ni maeneo gani ya kiutalii yatakayotembelewa.

Wasomi wa Kiafrika katika mazungumzo
1000+
Wajumbe Wanaotarajiwa
35+
Nchi Zilizowakilishwa
10
Wazungumzaji Wakuu
200+
Mawasilisho ya Utafiti
Mada Kuu

"Kiswahili na Lugha Nyingine Afrika: Mustakabali wa Ndani na Nje ya Mipaka ya Darasa katika Dunia Inayobadilika."

Mada za Kongamano

Mikondo ya Mazungumzo

 

01

Nafasi ya Kiswahili na Lugha Nyingine Afrika na Kwingineko katika Ushindani wa Kimataifa.

02

Matumizi ya Kiswahili katika Jamii: Nyumbani, Kazini, Biashara na Huduma za Kijamii.

03

Vyombo vya Habari, Mitandao ya Kijamii, na Maudhui ya Dijitali katika Kupanua Matumizi ya Kiswahili.

04

Vijana, Ubunifu, na Mabadiliko ya Kiswahili.

05

Kiswahili na Lugha nyingine: Ushirikiano, Ushindani, na Mustakabali wake.

06

Nafasi ya Kiswahili katika Sera na Utawala wa Lugha Barani Afrika na Kimataifa: Mchango na haja ya kuwa na Asasi za Kiswahili.

07

Kiswahili kama Nyenzo ya Uchumi na Ujasiriamali.

08

Ufundishaji wa Kiswahili Ndani na Nje ya Mfumo Rasmi wa Elimu: Fursa na Changamoto.

09

Kiswahili na Diaspora: Utambulisho, Uhamiaji, na Urithi wa Lugha.

10

Kiswahili katika Sanaa, Tafsiri, na Ukalimani: Fasihi, Muziki, Filamu, na Mawasiliano ya Lugha.

Tarehe Muhimu

Tenga Tarehe Hii

  1. Hatua 1
    3 Juni 2026
    Mwito wa Ikisiri
  2. Hatua 2
    20 Julai 2026
    Makataa ya Mwito wa Ikisiri
  3. Hatua 3
    30 Septemba 2026
    Taarifa ya Kukubaliwa
  4. Hatua 4
    31 Oktoba 2026
    Mwisho wa Usajili wa Mapema
  5. Hatua 5
    10–13 Disemba 2026
    Kongamano katika Chuo Kikuu cha Makerere
Wazungumzaji Wakuu

Sauti za Kitaaluma.

Tazama wote
Dkt. Anne Jebet
Dkt. Anne Jebet
Chuo Kikuu cha Virginia · Marekani
Kiswahili XXXXXX
Dkt. Filipo Lubua
Dkt. Filipo Lubua
Chuo Kikuu cha Pittsburg · Marekani
Teknolojia xxxxxxxx
Prof. Iribe Mwangi
Prof. Iribe Mwangi
Chuo Kikuu cha Nairobi · Kenya
Kiswahili Kuvuka Mipaka
Dkt. Hadija Jilala
Dkt. Hadija Jilala
Chuo Kikuu Huria · Tanzania
Mustakabali wa Lugha za Kiafrika
Ramani ya Uganda

Karibu Kampala. Karibu CHAUKIDU.

Jiunge na jumuiya ya kimataifa iliyojitolea kwa mustakabali wa Kiswahili na lugha za Kiafrika.